Jumapili 21 Septemba 2025 - 11:57
Hauli ya Marehemu Sheikh Abdallah Seifu yafanyika Mnang'ole Lindi

Hawza/ Hauli ya aliekuwa Sheikh wa kwanza wa Jumuiya ya Shia Ithnaasharia Tanzania (TIC), Hayati Sheikh Abdallah Seifu Linganaweka Imefanyika jana Jumamosi kijijini kwake Mnong'ole Lindi.

Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithnaasharia Tanzania Samaahat Sheikh Hemedi Jalala Mwakindenge, jana jumamosi akiambatana na jopo zima la Jumuiya ya Shia Ithnaasharia Tanzania (TIC), pamoja na walimu na wanafunzi wa Hawza ya Imaam Sw'adiq (as), walihudhuria kwenye Hauli ya Hayati Sheikh Abdallah Seifu Linganaweka (ra), iliyofanyika kijijini kwake Lindi.

Akizungumza na wakazi wa  kijiji cha Mnang’ole Lindi, katika Hauli hiyo ambayo iliambatana na hafla ya Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w), Sheikh Jalala alielezea historia ya Marehemu Samaahat Sheikh Abdallah Seifu (ra), ukarimu aliokuwa nao na jinsi gani alikuwa tayari kujitolea katika masuala ya kijamii.

Picha za tukio hilo ni kama ifuatavyo:

Hauli ya Marehemu Sheikh Abdallah Seifu yafanyika Mnang'ole Lindi

Hauli ya Marehemu Sheikh Abdallah Seifu yafanyika Mnang'ole Lindi

Hauli ya Marehemu Sheikh Abdallah Seifu yafanyika Mnang'ole Lindi

Hauli ya Marehemu Sheikh Abdallah Seifu yafanyika Mnang'ole Lindi

Hauli ya Marehemu Sheikh Abdallah Seifu yafanyika Mnang'ole Lindi

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha